Thursday, November 19, 2009

Wameshinda.

Kesho (Novemba 20 2009) mkataba wa “Soko la Pamoja” utasainiwa. Mkataba huo kikweli ndio shirikisho lenyewe la Afrika Mashariki. Kwa sisi wananchi tusio na madaraka ambao hatuoni mantiki ya Tanzania kujidumbukiza humo, lipi la zaidi tunaloweza kufanya? Binafsi ‘natundika daluga’ — wameshashinda — si salama tena kuzungumzia zaidi suala hili.

Posted by Mlenge in 11:50:07 | Permalink | No Comments »

Monday, March 9, 2009

‘Watanzania wana akili lakini hawazitumii’

Februari 11 2009, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania limetoa kauli kwamba “Watanzania wana akili lakini hawazitumii”, kwa mujibu wa taarifa ya gazeti la Tanzania Daima.

“Tuna mapori yenye rutuba, misitu, mabonde, mito, maziwa, bahari, milima na madini ya kila aina. Tusipoyatolea jasho kwa kufanya kazi, yatabaki hivyo hivyo, nasi tutaendelea kulalamika juu ya umaskini,” lilisema tamko hilo.

Kwa mujibu wa tamko hilo, Watanzania wana nguvu ambazo hazitumiki au zinatumika bila maarifa.

– Kauli ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania. Februari 11, 2009. Kama ilivyonukuliwa na gazeti la Tanzania Daima.

Kwa mujibu wa Wahashamu Maaskofu walioandika taarifa hiyo, akiwemo Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Watanzania wanatumia akili walizonazo kufanya mipango mibovu na hivyo kuiuza nchi kwa wajanja.

Posted by Mlenge in 05:01:15 | Permalink | No Comments »

Friday, October 31, 2008

Utumwa!

Sosholojia ya Utumwa
Posted by Mlenge in 11:44:47 | Permalink | No Comments »

Saturday, July 12, 2008

Tanzania ni nchi au siyo nchi?

Wiki ya kwanza ya Julai 2008 pamekuwa na mjadala Bungeni iwapo Zanzibar ni nchi au iwapo Zanzibar siyo nchi. Swali kama hili limeshapata kupelekwa mahakamani kuuliza iwapo Zanzibar ni dola au siyo dola.

Kwa kusaini mkataba wa Eac, Tanzania itakuwa siyo nchi. Haitakuwa dola wala shilingi! Haitakuwa Jamhuri. Na wala fursa ya kuulizana swali kama hilo la Zanzibar haitakuwepo! Ndio mkataba wa Eac ambao watawala wetu wamesaini.

Posted by Mlenge in 09:48:42 | Permalink | No Comments »

Saturday, May 31, 2008

Ahem!

Yaliyokuwamo kwenye Mtandao Huu yamechapishwa kama kitabu:
Mtandao Huu Unapumzishwa kwa Muda Usiojulikana.
*******

Hivi karibuni, magazeti ya Tanzania yameripoti kuhusu watu wa Pemba kutaka kujitenga. Suala hilo limeripotiwa na magazeti hayohayo kwamba limepokelewa kwa ukali na serikali. Angalau inatia matumaini kwamba kumbe serikali bado inapenda kuona Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kuwepo.., japo inatakiwa kuangalia kwa makini utatuzi wa “mpasuko” wa upande fulani Jamhuri ya Muungano. Swali linalokosa jibu la haraka, ni kwa nini “ukali” huo hauelekezwi kwa kufuta Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kunakopitia mikataba ya EAc? Au “ugomvi” wa serikali ni ile “namna” ya ufutwaji wa Jamhuri, na siyo “iwapo” Jamhuri inafutwa?
Posted by Mlenge in 14:05:55 | Permalink | No Comments »

Friday, April 11, 2008

Muungano wa Tanzania

Muungano wa Tanzania unakaribia miaka hamsini. Mikakati ipo kweli ya kuufikisha muungano huo miaka mia mbili ijayo?
Posted by Mlenge in 16:18:50 | Permalink | No Comments »

Monday, March 31, 2008

Ee Mungu, Nithibitishe kuwa ni Mpotofu!

Wakati Wamarikani wanataka kurusha chombo cha Anga za Juu kiitwacho “Challenger”, wahandisi walishauri kisirushwe kwa vile hali ya hewa ya baridi kali iliyokuwepo ingesababisha maafa. Lakini wale Wakurugenzi watoa maamuzi ya mwisho, waliamua kuwapuuza wale wahandisi, kwa vile walikuwa na mashinikizo ya kisiasa ya kuhakikisha chombo cha “Challenger” kinarushwa kwenda anga za juu haraka.

Wakati maandalizi yanaendelea ya kurusha chombo cha “Challenger”, wale wahandisi waliomba sala hii, “Ee Mungu, Tuthibitishe kuwa ni wapotofu” kwamba yale waliyo na hakika nayo kuwa chombo “Challenger” kitakutwa na dhoruba, yawe potofu. (“Ooh God! Prove us wrong!).

Ni sala hii niiombayo kwa kutazama Eac na hatima ya Tanzania — Ee Mungu, Nithibitishe kuwa na Mpotofu!

Mlenge

Posted by Mlenge in 16:11:26 | Permalink | No Comments »

Friday, February 29, 2008

Bunge la Tanzania

Mwezi huu wa Februari, Bunge la Tanzania lilileta matumaini mapya kwa wengi miongoni mwa Watanzania. Katika Bunge hilo, Waziri Mkuu Edward Lowassa alijiuzulu, na baraza jipya la Mawaziri kuundwa.  Wakati wakiapishwa kushika nyadhifa zao, Waheshimiwa Mawaziri hao walionekana wakila kiapo cha “kuitetea, kuilinda na kuihifadhi Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyowekwa kwa mujibu wa Sheria”. Lakini suala la Tanzania kuwemo kwenye Jumuia ya Afrika Mashariki ni ukiukwaji wa moja kwa moja wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyowekwa kwa mujibu wa Sheria.
Posted by Mlenge in 06:23:11 | Permalink | No Comments »

Tuesday, January 15, 2008

Hii vilevile ikumbukwe…

2. Isn’t EAC a brainchild project of EU? Will EU tell us to unite so that
we fight them? Is this the kind of “unity” Africa wants?

3. Tanzania is a member country of a big grouping SADC (population > 200m,
www.sadc.int). Kenya and Uganda are members of a bigger group IGAD
(population > 200m, www.igad.org). Aren’t these organisation existing in
the world that require unity? Don’t they reflect African Unity? Or their
“sin” is because they are linked to liberation struggle against
colonialism and imperialism; and were not established “under auspices” of
the West?

The sooner Tanzania pulls out of EAC, the better. Long live sovereign,
independent Tanzania.

Kind regards,

Mlenge

Posted by Mlenge in 12:10:28 | Permalink | Comments (2)

Nayo hii ikumbukwe…

1. EAC is not a larger unity: SADC and IGAD have history and numbers than
EAC. EAC is disunity (utengano) from bigger and established groupings of
SADC and IGAD. EAC cannot justifiably use “unity” as its selling point.

2. Because EAC is a brainchild of EU and the West; it is fallacious to
accept it just because our African countries were mapped out by the same
West. EAC does not represent Tanzania interests. Mission of IGAD and of
SADC are all gearing towards “Regional Integration”. Unlike EAC, IGAD and
SADC are genuine in their quest. EAC is a syndicate against Tanzania.
Tanzania is the “mbuzi wa shughuli” in EAC. It is OK to dissolve EAC or
for Tanzania to pull out of it soonest. Isn’t it? Why is it that very few
(if any) want to take blame / credit for dragging Tanzania to EAC hell.
[Am compiling the "EAC Hall of Fame/Shame(depending on how you look at
it)", listing all individuals who have openly supported the EAC Federation
with Tanzania being part of it. Can I add your name, Sir?]

Posted by Mlenge in 12:03:41 | Permalink | No Comments »