Thursday, November 19, 2009

Wameshinda.

Kesho (Novemba 20 2009) mkataba wa “Soko la Pamoja” utasainiwa. Mkataba huo kikweli ndio shirikisho lenyewe la Afrika Mashariki. Kwa sisi wananchi tusio na madaraka ambao hatuoni mantiki ya Tanzania kujidumbukiza humo, lipi la zaidi tunaloweza kufanya? Binafsi ‘natundika daluga’ — wameshashinda — si salama tena kuzungumzia zaidi suala hili.

Posted by Mlenge in 11:50:07 | Permalink | Comments Off

Monday, March 9, 2009

‘Watanzania wana akili lakini hawazitumii’

Februari 11 2009, Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania limetoa kauli kwamba “Watanzania wana akili lakini hawazitumii”, kwa mujibu wa taarifa ya gazeti la Tanzania Daima.

“Tuna mapori yenye rutuba, misitu, mabonde, mito, maziwa, bahari, milima na madini ya kila aina. Tusipoyatolea jasho kwa kufanya kazi, yatabaki hivyo hivyo, nasi tutaendelea kulalamika juu ya umaskini,” lilisema tamko hilo.

Kwa mujibu wa tamko hilo, Watanzania wana nguvu ambazo hazitumiki au zinatumika bila maarifa.

– Kauli ya Baraza la Maaskofu Katoliki Tanzania. Februari 11, 2009. Kama ilivyonukuliwa na gazeti la Tanzania Daima.

Kwa mujibu wa Wahashamu Maaskofu walioandika taarifa hiyo, akiwemo Mwadhama Polycarp Kardinali Pengo, Watanzania wanatumia akili walizonazo kufanya mipango mibovu na hivyo kuiuza nchi kwa wajanja.

Posted by Mlenge in 05:01:15 | Permalink | Comments Off

Friday, October 31, 2008

Utumwa!

Sosholojia ya Utumwa
Posted by Mlenge in 11:44:47 | Permalink | Comments Off

Saturday, July 12, 2008

Tanzania ni nchi au siyo nchi?

Wiki ya kwanza ya Julai 2008 pamekuwa na mjadala Bungeni iwapo Zanzibar ni nchi au iwapo Zanzibar siyo nchi. Swali kama hili limeshapata kupelekwa mahakamani kuuliza iwapo Zanzibar ni dola au siyo dola.

Kwa kusaini mkataba wa Eac, Tanzania itakuwa siyo nchi. Haitakuwa dola wala shilingi! Haitakuwa Jamhuri. Na wala fursa ya kuulizana swali kama hilo la Zanzibar haitakuwepo! Ndio mkataba wa Eac ambao watawala wetu wamesaini.

Posted by Mlenge in 09:48:42 | Permalink | Comments Off

Saturday, May 31, 2008

Ahem!

Yaliyokuwamo kwenye Mtandao Huu yamechapishwa kama kitabu:
Mtandao Huu Unapumzishwa kwa Muda Usiojulikana.
*******

Hivi karibuni, magazeti ya Tanzania yameripoti kuhusu watu wa Pemba kutaka kujitenga. Suala hilo limeripotiwa na magazeti hayohayo kwamba limepokelewa kwa ukali na serikali. Angalau inatia matumaini kwamba kumbe serikali bado inapenda kuona Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kuwepo.., japo inatakiwa kuangalia kwa makini utatuzi wa “mpasuko” wa upande fulani Jamhuri ya Muungano. Swali linalokosa jibu la haraka, ni kwa nini “ukali” huo hauelekezwi kwa kufuta Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kunakopitia mikataba ya EAc? Au “ugomvi” wa serikali ni ile “namna” ya ufutwaji wa Jamhuri, na siyo “iwapo” Jamhuri inafutwa?
Posted by Mlenge in 14:05:55 | Permalink | Comments Off

Friday, April 11, 2008

Muungano wa Tanzania

Muungano wa Tanzania unakaribia miaka hamsini. Mikakati ipo kweli ya kuufikisha muungano huo miaka mia mbili ijayo?
Posted by Mlenge in 16:18:50 | Permalink | Comments Off

Monday, March 31, 2008

Ee Mungu, Nithibitishe kuwa ni Mpotofu!

Wakati Wamarikani wanataka kurusha chombo cha Anga za Juu kiitwacho “Challenger”, wahandisi walishauri kisirushwe kwa vile hali ya hewa ya baridi kali iliyokuwepo ingesababisha maafa. Lakini wale Wakurugenzi watoa maamuzi ya mwisho, waliamua kuwapuuza wale wahandisi, kwa vile walikuwa na mashinikizo ya kisiasa ya kuhakikisha chombo cha “Challenger” kinarushwa kwenda anga za juu haraka.

Wakati maandalizi yanaendelea ya kurusha chombo cha “Challenger”, wale wahandisi waliomba sala hii, “Ee Mungu, Tuthibitishe kuwa ni wapotofu” kwamba yale waliyo na hakika nayo kuwa chombo “Challenger” kitakutwa na dhoruba, yawe potofu. (“Ooh God! Prove us wrong!).

Ni sala hii niiombayo kwa kutazama Eac na hatima ya Tanzania — Ee Mungu, Nithibitishe kuwa na Mpotofu!

Mlenge

Posted by Mlenge in 16:11:26 | Permalink | Comments Off

Friday, February 29, 2008

Bunge la Tanzania

Mwezi huu wa Februari, Bunge la Tanzania lilileta matumaini mapya kwa wengi miongoni mwa Watanzania. Katika Bunge hilo, Waziri Mkuu Edward Lowassa alijiuzulu, na baraza jipya la Mawaziri kuundwa.  Wakati wakiapishwa kushika nyadhifa zao, Waheshimiwa Mawaziri hao walionekana wakila kiapo cha “kuitetea, kuilinda na kuihifadhi Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyowekwa kwa mujibu wa Sheria”. Lakini suala la Tanzania kuwemo kwenye Jumuia ya Afrika Mashariki ni ukiukwaji wa moja kwa moja wa Katiba ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania iliyowekwa kwa mujibu wa Sheria.
Posted by Mlenge in 06:23:11 | Permalink | Comments Off

Tuesday, January 15, 2008

Ikumbukwe nayo ilisemwa…

Just because “Umoja ni nguvu” you do not just unite with anybody. In
Hitler’s Europe talking “integration” would not make much sense. Would it?
Actually EAC defeats the purpose of “umoja ni nguvu” because EAC is
“utengano” from bigger, well-established organisations; namely, IGAD and
SADC.

Hitler and Nazi, like many other rulers, were elected by people. Should we
put WWII “Blitzkrieg” blame on the Germany people because they
democratically electing Hitler before he declared his “Third Reich”? Was
Hitler representing the will of the people? Again, suggesting that because
Kikwete is from CCM;  Mkapa was also from CCM; and Wananchi have elected
Kikwete of Mkapa’s CCM, therefore Wananchi have accepted all that Mkapa
did, including EAC:– such kind of argument is a classical “ad hominem”
fallacy.

* CCM Manifesto does not agree to surrender Tanzania’s sovereignty to a
wilaya/mkoa of EAC, or anybody.

* Overwhelming majority of Tanzanians (80%) reject the over-hyped EAC
(http://allafrica.com/stories/200704290112.html).

If we have not, as a country, lost our sanity, then we should listen to
the voice of majority (“Sauti ya Watu Wengi ni Sauti ya Mungu” — msemo wa
Kiswahili)

Mlenge

Posted by Mlenge in 12:00:53 | Permalink | Comments Off

Ikumbukwe tu ilishasemwa…

Wizara [inayohusika na sheria na katiba] itoe Waraka wa Serikali wa Kuongeza kanuni zifuatazo kwenye uendeshaji wa Kesi za Jinai na za Madai:

1. Kabla ya Kumtia Hatiani Mshtakiwa Yoyote, akabidhiwe nakala ya Mwenendo wa Kesi. Kabla ya Kutolewa Hukumu yoyote, Mshtakiwa apewe nakala ya Mwenendo wa Kesi.

2. Hukumu inapotolewa kwa Kesi yoyote, Mshtakiwa apewe PAPO HAPO nakala ya Hukumu. Kwa mshitakiwa asiyeona, mwenendo wa Kesi, pamoja na Hukumu viwe kwa maandishi maalum ya wasioona.

3. Kama Mshitakiwa atatiwa hatiani pasipo kupewa nakala ya mwenendo wa Kesi KABLA ya kutiwa hatiani, hatia hiyo isitambuliwe kisheria.

4. Kama mshtakiwa yoyote atahukumiwa pasipo kukabidhiwa nakala ya Hukumu PAPO HAPO, basi Hukumu hiyo ihesabiwe kuwa ni batili, isipokuwa pale mtu anaposhitakiwa pasipo kuwepo Mahakamani, ambapo itamlazimu Mtoa Hukumu kuiweka Nakala ya Hukumu hiyo tayari.

5. Muda wa Mahabusu uhesabiwe kwenye kifungo [Mahabusi zina hali mbaya zaidi kuliko hata magereza!, au, Mahabusu wana hali mbaya zaidi kuliko Wafungwa!] Mtu anayekaa Mahabusu kwa Muda unaofikia Kiwango cha Chini cha Adhabu, Aachiliwe Huru, na kesi yake ifutwe. Mtu anayekaa mahabusu Miaka Kadhaa, Halafu akahukumiwa kwenda Jela Miaka Kadhaa+Miaka Kadha wa Kadha, basi atakaa jela Miaka Kadha wa Kadha tu, kwa vile ashakaa Mahabusu miaka kadhaa.

6. Kwa kosa lolote lenye adhabu ya Kifungo cha zaidi ya Miaka Mitano (5), Rufaa iwe ni \’automatic\’ — Mshitakiwa hahitaji kufanya lolote ili kesi yake iangaliwe na Mahakama ya Juu zaidi… Labda kama Mshitakiwa mwenyewe atasema bayana hataki Rufaa. [Ufaransa ni moja ya nchi zifanyazo hivyo]

7. Kanuni ya Adhabu itamke kwamba “Kifungo cha Maisha” maana yake ni “Miaka 15 Jela”. Adhabu zote zinazozidi Miaka 15 zipunguzwe na kuwa kuwa “Kifungo cha Maisha” au, vizuri zaidi, cha chini ya hapo. [Sweden hufanya hivi pia]

8. Pawepo na “Automatic Parole” kwa vifungo. Labda tuseme 60% ya kifungo itakuwa gerezani, na 40% itakuwa ya “parole”, labda isipokuwa mfungwa atakuwa anatumikia pia adhabu nyingine muda huo wa ‘parole‘.

“Ukitaka kujua watu ni binadamu kiasi gani, tembelea magereza yao!” — Nukuu

Posted by Mlenge in 11:52:10 | Permalink | Comments Off