Yaliyokuwamo kwenye Mtandao Huu yamechapishwa kama kitabu:
Mtandao Huu Unapumzishwa kwa Muda Usiojulikana.
*******
Hivi karibuni, magazeti ya Tanzania yameripoti kuhusu watu wa Pemba kutaka kujitenga. Suala hilo limeripotiwa na magazeti hayohayo kwamba limepokelewa kwa ukali na serikali. Angalau inatia matumaini kwamba kumbe serikali bado inapenda kuona Jamhuri ya Muungano wa Tanzania inaendelea kuwepo.., japo inatakiwa kuangalia kwa makini utatuzi wa “mpasuko” wa upande fulani Jamhuri ya Muungano. Swali linalokosa jibu la haraka, ni kwa nini “ukali” huo hauelekezwi kwa kufuta Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kunakopitia mikataba ya EAc? Au “ugomvi” wa serikali ni ile “namna” ya ufutwaji wa Jamhuri, na siyo “iwapo” Jamhuri inafutwa?